Na Mwandishi Wetu
BENDI ya muziki wa dansi Extra Bongo Next Level imeungana na familia na wanahabari wote nchini kuomboleza kifo cha Mhariri wa Habari za Michezo wa gazeti la Mtanzania Rachel Mwiligwa kilichotokea usiku wa kuamkia Ijumaa.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa bendi hiyo, 'Kamarade' Ally Choki, Extra Bongo imepokea kwa mshituko taarifa za kifo cha Rachel kutokana na kutambua na kuthamini mchango wake alioukuwa akiutoa katika harakati zake za kupigania kurudisha ushindani wa muziki wa dansi kama ilivyokuwa miaka ya nyuma.
Alisema, wanatoa pole kwa familia yake, waandishi wa habari za michezo na wafanyakazi wenzake wote, wasanii na wanamichezo wengine katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na mdau mkubwa wa michezo na burudani.
Akimwelezea marehemu, Choki, alisema, Recho alikuwa mdau mkubwa wa bendi hiyo na alishiriki kuasisi Extra Bongo TP Sunday bonanza akishirikiana na baadhi ya waandishi wa habari za burudani kwa lengo la kuinua kiwango chao kimuziki hatua ambayo iliwaletea tija.
Alisema, Rachel, alishiriki kwa kiwango kikubwa kutoa ushauri wa kiufundi ndani na nje ya bendi na kutumia kalamu yake pia kuilezea vyema Extra Bongo hivyo ni vigumu kwa familia ya bendi hiyo kumsahau ambapo wanatarajia kuwasilisha rambirambi kwa familia ya marehemu kwa kushirikiana na Kamati ya mazishi.
mwisho.
MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA
1. Wahiraki, Hawa ni wanawake wa jamii ya Wahiraki wa napatikana kaskazini mwa Tanzania wamezagaa mikoa ya manyara ni weupe Wana Umbo zuri wanavutia kwa Macho. 2. Warangi, Hawa ni wanawake jamii ya Warangi ni wazuri nywele zao ni asili ya waraabu weupe sura nzuri wanapatikana kondoa. 3. Wanyiramba. Hawa ni warembo Sana sura matata wanapatikana mkoa wa singida kaskazini, usipokua makini utawafananisha na wanyaturu 4. Wamasai, kabila hili wanawake wazuri sio wengi Sana lakini ukikutana na sampuli Tatu au nne hivi utauza hata boxa kuongezea mahari wamezagaa Sana Arusha 5. Wahaya, hawa nao ni jamii ya Kanda ya ziwa maumbile Yao Kuna weupe miguu Yao ya bia shape matata wamejaa Sana bukoba. 6. Wanyaturu, Hawa wanafanana na Wanyiramba wanapatikana singida hasa ikungi na manyoni weupe wanavutia 7. Wapare, Hii ni jamii ya kabila la Wapare wanapatikana moshi wilaya ya same wako vizuri usicheze kabisa na hili kabila shape nzuri. 8 .Wamakonde, Hawa wanapatikana kusini mwa Tanzania ni kab
Comments