Baadhi ya wageni waalikwa wakiwa kwenye foleni ya kuingia Ikulu, Dar es Salaam leo, kwenda kushuhudia wakati Rais Jakaya Kikwete akiwaapisha mawaziri wapya na waliobadilishwa wizara. |
Rais Jakaya Kikwete (kushoto) akimwapisha Shgmasi Vuai Nahodha kuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
JK akimwapisha Dk. Husein Mwinyi kuwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii
JK akimkabidhi zana za kazi, Waziri wa Maji, Profesa Jumanne Maghembe
JK akimwapisha Hawa Ghasia kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Tawla za Mikoa na Serikali za Mitaa
Jk akimkabidhi zana za kufanyia kazi, Waziri wa Utawala Bora, George Mkuchika |
Waziri mpya wa Mambo ya Ndani, Emmanuel Nchimbi, akila kiapo cha koshika wadhifa huo
Mbunge wa Mvomero, Amos Makalla akila kiapo mbele ya JK cha Unaibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Waziri wa Maji, Prof. Maghembe (kulia) na Waziri mpya wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Christopher Chizza.
Makamu wa Rais, Dk. Mohamed Gharib Bilal akimpongeza Naibu Waziri wa Fedha, Janet Mbene
Aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja (kushoto) akimpongeza January Makamba ambaye ni Naibu Waziri wa Sayansi, Teknolojia na Mawasiliano.
Naibu Waziri wa Fedha, Janet Mbene akiteta na Naibu Waziri wa Nisharti na Madini, Steven Masele
Rais Jakaya Kikwete (mstari wa mbele katikati) Makamu wa Rais, Dk. Bilal (kulia kwake) na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda (kushoto kwake) wakiwa katika picha ya pamoja na mawazi na Naibu mawaziri walioapishwa leo
JK akiwa katika picha ya pamoja na mawaziri walioapishwa leo
JK na naibu mawaziri walioapishwa leo
Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe (kushoto) akizungumza na Nibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Phillip Mulugo. Wote hao wanatokea Mkoa wa Mbeya.
Comments