KIM:SIKUTEUA WACHEZAJI STARS KWA UPENDELEO


KOCHA wa Taifa Stars Kim Poulsen amekana kupendelea katika uteuzi wa wachezaji wa kikosi hicho  na kusema kwamba alichagua wachezaji kutokana uwezo na sifa walizonazo na si kuangalia ni mchezaji wa timu gani.
 
Alisema nashangazwa na maalalamiko ya baadhi ya wadau wa soka ambao wamekuwa wakielekeza shutuma hizo ambazo hazina ukweli wowote. 
 
Baadhi ya wadau walimekuwa wakimlalamikia kocha huyo kutokana na kuchagua nyota wengi kwenye kikosi hicho wakitokea klabu ya Simba huku mahasimu wao Yanga, akiteua mchezaji mmoja tu.
 
Aliongeza kuwa kikosi chake ambacho kinajiandaa na mchezo wake wa kuwania kombe la Dunia dhidi ya Ivory Coast kitaenda bila ya nyota wake Nurdin Bakari na Thomas Ulimwenguni ambao walipata majeruhi wakati wa mazoezi yao na kusema kuwa watabaki wakijinoa kabla ya kuungana na wenzao watakaporudi ili kujiandaa.
Akizungumzia mchezo wao dhidi ya Ivory Coast utakaopigwa juni 2 huko Abdjan, Paulsen alisema  kikosi chake kinaiheshimu kutokana na kuwa na wachezaji nyota wengi wenye  uwezo kisoka kwa ambao wanacheza ligi za ulaya wakiwemo  Didier Dragba, Solomon Kalou, Yaya Toure, Kolo Toure na wengineo. 
 
Alisema pamoja na hilo hawaiogopi zaidi ya kuwataka wachezaji wa Stars kutambua hawana tofauti na Ivory Cost isipokuwa ni mbinu tu za hapa na pale ambazo anaamini kwa uwezo walichonacho wachezaji wa Stars wanaweza kushinda.na mechi yao dhidi ya Gambia.

Wachezaji wengine waliopo Stars ni pamoja na  makipa; Juma Kaseja (Simba), Mwadini Ally (Azam) na Deogratius Munishi (Mtibwa Sugar). Mabeki: Nassor Masoud Cholo (Simba), Aggrey Morris (Azam), Amir Maftah (Simba), Erasto Nyoni (Azam), Kelvin Yondani (Simba), Waziri Salum (Azam), Shomari Kapombe (Simba) na Juma Nyoso (Simba).
 
Viungo ni Mwinyi Kazimoto (Simba), Salum Abubakar (Azam), Jonas Mkude (Simba), Shabani Nditi (Mtibwa Sugar), Edward Christopher (Simba- U20), Mrisho Ngasa (Azam) na Frank Domayo (JKT Ruvu- U20).
 
Washambuliaji ni Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo), Ramadhan Singano (Simba-U20), Simon Msuva (Moro United- U20),  Haruna Moshi (Simba) na John Bocco (Azam). Chanzo Mama Pipilo Blog

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI