KIM:SIKUTEUA WACHEZAJI STARS KWA UPENDELEO
KOCHA wa Taifa Stars Kim Poulsen amekana kupendelea katika uteuzi wa wachezaji wa kikosi hicho na kusema kwamba alichagua wachezaji kutokana uwezo na sifa walizonazo na si kuangalia ni mchezaji wa timu gani.
Alisema nashangazwa na maalalamiko ya baadhi ya wadau wa soka ambao wamekuwa wakielekeza shutuma hizo ambazo hazina ukweli wowote.
Baadhi ya wadau walimekuwa wakimlalamikia kocha huyo kutokana na kuchagua nyota wengi kwenye kikosi hicho wakitokea klabu ya Simba huku mahasimu wao Yanga, akiteua mchezaji mmoja tu.
Aliongeza kuwa kikosi chake ambacho kinajiandaa na mchezo wake wa kuwania kombe la Dunia dhidi ya Ivory Coast kitaenda bila ya nyota wake Nurdin Bakari na Thomas Ulimwenguni ambao walipata majeruhi wakati wa mazoezi yao na kusema kuwa watabaki wakijinoa kabla ya kuungana na wenzao watakaporudi ili kujiandaa.
Akizungumzia mchezo wao dhidi ya Ivory Coast utakaopigwa juni 2 huko Abdjan, Paulsen alisema kikosi chake kinaiheshimu kutokana na kuwa na wachezaji nyota wengi wenye uwezo kisoka kwa ambao wanacheza ligi za ulaya wakiwemo Didier Dragba, Solomon Kalou, Yaya Toure, Kolo Toure na wengineo.
Wachezaji wengine waliopo Stars ni pamoja na makipa; Juma Kaseja (Simba), Mwadini Ally (Azam) na Deogratius Munishi (Mtibwa Sugar). Mabeki: Nassor Masoud Cholo (Simba), Aggrey Morris (Azam), Amir Maftah (Simba), Erasto Nyoni (Azam), Kelvin Yondani (Simba), Waziri Salum (Azam), Shomari Kapombe (Simba) na Juma Nyoso (Simba).
Viungo ni Mwinyi Kazimoto (Simba), Salum Abubakar (Azam), Jonas Mkude (Simba), Shabani Nditi (Mtibwa Sugar), Edward Christopher (Simba- U20), Mrisho Ngasa (Azam) na Frank Domayo (JKT Ruvu- U20).
Washambuliaji ni Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo), Ramadhan Singano (Simba-U20), Simon Msuva (Moro United- U20), Haruna Moshi (Simba) na John Bocco (Azam). Chanzo Mama Pipilo Blog
Comments