THE
UNITED REPUBLIC
OF TANZANIA
DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512,
2116898
E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com
Fax: 255-22-2113425 |
|
PRESIDENT’S OFFICE,
THE
STATE HOUSE,
P.O. BOX
9120,
DAR
ES SALAAM.
Tanzania.
|
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
KUAPISHWA
KWA MAWAZIRI NA NAIBU MAWAZIRI
Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania,
Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, atawaapisha Mawaziri na Naibu Mawaziri Jumatatu tarehe 7 April, 2012, saa 5 asubuhi
katika viwanja vya Ikulu.
Kwa kuzingatia umuhimu wa
shughuli hii, Nawaomba wahariri mtutumie
majina ya waandishi waandamizi ambao watafika ikulu mapema saa 4.00 asubuhi kwa
ajili ya shughuli hii.
Tunaomba majina hayo ya
wawakilishi wa vyombo vyenu yawasilishwe kwetu mara baada ya kupata taarifa hii na mwisho wakupokea majina itakuwa saa 2.00 asubuhi ya Jumatatu, kwa sababu ifikapo
saa 4.00 kamili asubuhi kila mwalika anatakiwa awe tayari ameshakaa kwenye
sehemu yake aliyopangiwa.
Tunapenda kusisitiza kuwa
waandishi watakaoruhusiwa kuhudhuria shughuli hii ni wale tu ambao tutapokea
majina yao
kutoka kwa wahariri wa vyombo husika. Aidha, tunasisitiza mavazi yawe nadhifu
na heshima, kwa kuwa hii ni shughuli ya Kitaifa.
Tunaomba ushirikiano wenu na
karibuni.
……..Mwisho…..
Imetolewa na:
Kurugenzi
ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
5 Mei, 2012
Comments