MJUE MISS EAST AFRICA 2012

 Warembo watakaoziwakilisha Nchi zao katika mashindano ya Miss East Africa mwaka huu wanaendelea  kupatikana kutoka katika Nchi mbalimbali zinazoshiriki mashindano hayo.

Mrembo mwingine aliyeingia fainali ni Miss Lula Teklehaimanot (19) (pichani), kutoka Nchini Ethiopia ambae alipatikana mwishoni mwa wiki baada  ya kuwashinda warembo wenzake waliojitokeza kutaka kuiwakilisha Ethiopia katika fainali hizo.
 Miss Lula Teklehaimanot ana urefu wa 1.79m  na uzito wa 52kg ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza katika Chuo cha St. Merry University cha jijini Addis Ababa, Ethiopia ampapo anasomea Degree ya Marketing.

Pia Mrembo huyo ni miongoni mwa wanamitindo maarufu  wanaochipukia kwa kasi Nchini Ethiopia.

Fainali za mashindano ya Miss East Africa 2012 zitafanjika tarehe 07 mwezi September mwaka huu jijini Dar es salaam ambapo zitashirikisha Nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Somalia, Djibouti, Eritrea, Sudan, Ethiopia, Malawi, Madagascar, Reunion, Comoros, Seychelles, na Mauritius.

Mashindano ya Miss East Africa yanaandaliwa na kumilikiwa na kampuni ya Rena Events Ltd ya jijini Dar es salaam.Kwa hisani ya Daily Mitikas Blog

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA