TUME YA KURATIBU MAONI YA KATIBA MPYA YAKABIDHIWA OFISI KATIKA JENGO JIPYA LA WIZARA YA MAMBO YA NDANI
Katibu Mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue kushoto akimtembeza Mwenyekiti
wa Tume ya kuratibu maoni ya Katiba mpya Waziri mkuu mstaafu Jaji
Joseph Warioba katika ofisi mpya ya Tume hiyo iliyopo katika jengo
jipya la Wizara ya mambo ya Ndani ghorofa ya kwanza katika hafla ya
makabidhiano iliyofanyika leo kwenye Wizara ya mambo ya ndani jijini Dar
es salaam, katikati ni Celina Kombani Waziri wa Sheria na Katiba.
Katibu Mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue kushoto akimueleza jambo Mwenyekiti
wa Tume ya kuratibu maoni ya Katiba mpya Waziri mkuu mstaafu Jaji Joseph
Warioba wakati wa makabidhiano ya ofisi ya Tume hiyo iliyopo katika jengo jipya la
Wizara ya mambo ya Ndani ghorofa ya kwanza , wa pili kutoka kushotoni Celina
Kombani Waziri wa Sheria na Katiba na Angela Kairuki mbunge wa CCM viti maalum Dar es salaam
Ofisi inavyoonekana kwa ndani.
Mwenyekiti wa Tume ya Kuratibu maoni ya Katiba Mpya Waziri mkuu mstaafu
Jaji Joseph Wariomba wa tatu kutoka kulia akiwa pamoja na viongozi
wengine wakibadilishana mawazo kabla ya kuanza kwa hafla hiyo. Chanzo;Full shangwe Blog
Comments