UWABA yahamasisha wananchi kupanda baiskeli

Baadhi ya wapanda baiskeli katika matembezaji ya uhamasishaji upandaji wa baiskeli kama vyombo vingine vya usafiri, wakijitayarisha kupanda baiskeli zao zao kwa ajili ya matembezi hayo, Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam leo, kuelekea viwanja vya Biafra, Kinondoni na kurudi tena kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja. Matembezi hayo yaliandaliwa na Umoja wa Wapanda baiskeli Tanzania (UWABA) na kushirikisha watu wa rika mbalimbali. (Picha zote na Khamisi Mussa)


Waendesha baiskeli inayoendeshwa na watu wawili, Jeremy Yamin (mbele) na Alicia Yamin, wakiwa tayari kwa matembezi hayo, Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini.


Mgeni rasmi katika matembezi ya baiskeli, Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid, akisalimiana na Balozi wa Wapanda baiskeli duniani, Filberto Sebregondi (kushoto), wakati wa kuanza kwa matembezi hayo, yaliyokuwa yakihamasisha wananchi kupanda chombo hicho kwa ajili ya kuimarisha afya zao kimazoezi.



Mgeni rasmi katika matembezi ya baiskeli, Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid (wa pili kulia), akiwa Balozi wa Wapanda baiskeli duniani, Filberto Sebregondi (wa pili kushoto) pamoja na wapanda baiskeli wengine, wakiendesha baiskeli zao hizo kuelekea viwanja vya Biafra Kinondoni na kisha kurudi kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini.


Balozi wa Wapanda baiskeli duniani, Filberto Sebregondi, akiwa amepanda baiskeli ya mmoja wa washiriki wa matembezi hayo, baada ya kumvutia kutokana na mapambo yake.


Mpanda baiskeli kutoka Uingereza, Chris Morgan, akiwa amempakia mtoto wake kwenye basikeli kwa ajili ya matembezi hayo.




Msafari wa wapanda baiskeli, ukiongozw ana kijana aliyeuwa na ulemavu wa mguu mmoja, ukiwa njiani kuelekea Viwanja vya Biafra, Kinondoni jijini Dar es Salaam.


Msafara wa baadhi ya wapanda baiskeli, ukiwa na kijana wa miaka 5 (kulia), ukielekea kwenye viwanja hivyo kwa ajili ya kuhamasisha wananchi kupanda chombo hicho kwa ajili ya kufanya mazoezi ya kuimarisha afya zao.


Baadhi ya wananchi wenye ulemavu wakiendesha baiskeli zao kwa ajili ya kushiriki matembezi hayo ya kuhamasisha upandaji baiskeli kama vyombo vingine vya usafiri.

Mgeni rasmi katika matembezi ya baiskeli, Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid, akizungumza jambo na Balozi wa Wapanda baiskeli duniani, Filberto Sebregondi (kushoto), wakati wa matembezi hayo, maeneo ya Viwanja vya Biafra, Kinondoni.


Mgeni rasmi katika matembezi ya baiskeli, Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid, akizungumza jambo na Profesa Karim, wakati matembezi hayo ya baskeli yalipofika kwenye viwanja vya Biafra, Kinondoni.





Balozi wa Wapanda baiskeli duniani, Filberto Sebregondi, akizunguma na wapanda baiskeli, wakati walipomaliza matembezi hayo Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam leo.



Mgeni rasmi katika matembezi ya baiskeli, Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid, akizungumza na wapanda baiskeli wakati wa kumalizika matebezi hayo, Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam.


Mgeni rasmi katika matembezi ya baiskeli, Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid, akimkabidhi zawadi ya baiskeli, Desiberi Massawe baada ya kushinda katika bahati nasibu iliyochezeshwa viwanjani hapo, baada ya kumalizika matembezi hayo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*